Friday, May 29, 2020

WINNING IS ALL I DO

Assalamualaikum

      Leo naleta uzi utakaotembea kwa jina la WINNING IS ALL I DO hapa naelezea au kukuasa kutojihusisha na biashara ya wahuni wanajiita QNET, AIM GLOBAL pamoja na binamu zao. Hawa jamaa wamekuwa wakilaghai watu kwa kiwango kikubwa sana
       Ili nisikuchoshe mpendwa msomji wa ukurasa huu, twende chap chap kwenye uzi husika, iko hivi, hii biashara hujulikana kama e commerce yaaani electronic commerce, hii unanunua bidhaa mtandaoni yaani kwa internet
     Hawa jamaa wako na swagger zao fulani tamu sana,  utasikia ukiunganishwa na wewe ukaunganisha watu kadhaa unakuwa millionaire, leo nakuibia siri kama kweli unakuwa millionaire muone viatu vyake utakuta kanunuaga vile bibuti vya jeje na soli imeisha upande, jiulize yeye mbona hajawa millionaire?

  Watumishi wengi wa serikali hasa Sekta ya elimu(hapa nawazungumzia walimu wenzangu) wamekuwa wahanga wakubwa wa janga hili, yaani unakuta ka risk kama 1m hadi 4m huku akitarajia kuwa future millionaire na wanapenda kunifariji kwa kuitana ama wanapopeana hi utasikia Good morning millionaire
  
Pamoja na kuitana majina matamu yanayo sound vizuri, watu hawa ndo wanaongoza kwa mizinga kuliko hata Girl friend wako utasikia una buku hapo!

  Ukweli uko hivi, ukisha kuunganishwa na kutoa pesa ya kiingilio unatakiwa uunganishe watu almost 16 hii ni kama kuchanganua sentensi kwa njia ya matawi, walimu wenzangu wa kiswahili nafikiri hapa mnanielewa vilivyo, utakuta mtu anamiaka karibia 6 hadi 7 toka aunganishwe hajaunga hata mmoja au kaunga watatu na tayari ashajua kuwa aliingia mkenge lakini haachi kutafuta watu ili awachomeshe nao, hawa QNET, AIM GLOBAL, SIJUI ALLIANCE hawana tofauti na BAY PORT
Ukiwaona usiwasikilize, nakwambia usiwape nafasi ya kuwasikiliza kama F3 Response yako ni freeze mode umeisha mimi yangu ni fight mode hawaniwezi hata wakiungana

No comments:

Post a Comment

HISTORIA YA LUGHA Nadharia juu ya lugha ya kiswahili Kuna nadharia mbali mbali zinazoelezea asili ya lugha ya ...