Vivumishi ni maneno ambayo hutumiwa kutuelezea zaidi kuhusu nomino. Aghalabu,huja baada ya nomino.
Kuna aina kadhaa za vivumishi tutakazozungumzia:
i. Vivumishi vimilikishi
ii. Vivumishi vya sifa
iii. Vivumishi vya idadi
iv. Vivumishi visisitizi
v. Vivumishi viulizi
vi. Vivumishi vya ki-mfano
vii. Vivumishi vya a-unganifu
viii. Vuvumishi vionyeshi
VIVUMISHI VIMILIKISHI
• Vivumishi vimilikishi hutumika kuonyesha umiliki wa nomino kwa nyingine.
Mizizi yake huundwa kwa kutumia : -angu , -etu ,-ake , -ao na kadhalika ili kuonyesha umiliki. Mf. :Gari yangu ni nyekundu
VIVUMISHI VYA SIFA
Vivumishi hivi hutumika kutoa sifa ya nomino mbalimbali. Mf. : kali, chungu, safi, kubwa.
Tazama sentensi hii: Yule kijana mrefuana pua kubwa.
VIVUMISHI VYA IDADI
• Hutumiwa kueleza kuhusu idadi ya nomino.
• Yaweza kuwa ya aina mbili:
i. Idadi isiyodhihirika:kiasi cha nomino kinatajwa kwa ujumla.Mf:chache,wastani,nyingi.
ii. Idadi kamili:nambari hutumiwa kuelezea idadi ya nomino.Mf:kumi,mia,elfu.
K.m: Watu wengi waliabudu sanamu lakini watatu walikataa.
VIVUMISHI VISISITIZI
• Hutumiwa kusisitiza nomino fulani .Mf: yuyu huyu, kiki hiki, mumu humu.
• K.m : Mzee yuyu huyu mwenye nywele nyeupe amemwoa binti wa miaka 24.
VIVUMISHI VIULIZI
• hutumika kuuliza swali na hutumia viambishi vya ngeli. Mf: -pi?
• K.m : Jino lipi limeng’oka?
VIVUMISHI VYA KI- MFANO
• hulinganisha sifa ya nomino na hali au tabia nyingine.
• Hutanguliwa na nomino,a-unganifu na huchukua kiungo –ki. Mf.:Kijeshi, kifalme,kitajiri,kiafrika,kikazi
• K.m: Jakie anapenda kuvaa mavazi ya kiume
VIVUMISHI VYA A-UNGANIFU
• Hutuelezea zaidi kuhusu nomino kwa kuonyesha kitu kinachomiliki nomino hiyo.Mf.: la, ya, cha, za.
• Hkiambishi cha nafsi/ngeli huambatanishwa na kiambishi –a cha a-unganifu ,kisha nomino.
• K.m:Nguo za Daudi zilianguka alipocheza
VIVUMISHI VIONYESHI/VIASHIRIA
• Huashiria nomino kulingana na mahali.
• K.m:Huyu ni Peace, huyo ni Brian na yule ni Zubeda
No comments:
Post a Comment